MIC - DASH BONGO ALL NEWS
Hapa ni mahali zinapo patikana habari zote za kisiasa, burudani na michezo kutoka TANZANIA!!
Wednesday, August 3, 2016
WAJUE WASANII WATANO WA MUZIKI WA BONGO FLAVA WENYE UKWASI MKUBWA TANZANIA 2016
Saturday, July 2, 2016
BODI YA MIKOPO YAKANUSHA UKATA WA FEDHA
HESLB YAKANUSHA KUWA HAINA FEDHA
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu inapenda kukanusha taarifa za upotoshaji zinazoenezwa kwa sasa kwamba haina fedha.
Si kweli kwamba Bodi haina fedha, ila ni kweli kwamba kumekuwa na ucheleweshaji wa kufikisha fedha za wanafunzi vyuoni kutokana na zoezi la kuhakiki wanafunzi wanaonufaika na mikopo linaloendelea vyuoni hivo
Hata hivyo, maandalizi ya malipo hayo yameshafanyika na ‘pay sheets’ zimeshapelekwa vyuoni tayari kwa wanafunzi wanaonufaika na mikopo kusaini.
Bodi inatarajia wakati wowote wiki ijayo baada ya zoezi la uhakiki kukamilika; itapeleka fedha hizo vyuoni
IMETOLEWA NA:KITENGO CHA HABARI, ELIMU NA MAWASILIANO BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU TAREHE 2 JULAI 2016
Friday, July 1, 2016
CELEB WATANO WAKIKE WENYE UZURI WAKIPEKEE BONGO
5. JACQLINE NTUYABALIWE
Alikua miss tanzania wa zamani na kwa sasa ni Mke wa mfanya biashara maarufu hapa nchini tanzania na mama wa watoto wawili mapacha. Lakini pia ni mfanya biashara na mwana muziki wa nyimbo za bongo flaivor aliye wai kutamba na nyimbo inayo julikana kwa jina la "Nalia kwa furaha" aliyo mshirikisha msanii mwenzake bushoke. Anavutia since ni mama but ukikutana naye unaweza jua si mama wa watotowa wili.
4. VANESSA MDEE
huyu ni msanii wa bongo flavor ambaye ametamba nanyimbo kama "HAWAJUI" , "ME AND YOU" na nyinginezo nyingi! Ni mwenyeji wa mkoa wa Arusha. Anashikilia na fasi ya nne kutokana uzuri wa ngozi yake ambayo ni natural pamoja na Umbo lake dogo dogo ambalo ni so ameizing sanaa since kila mtupio anao utupia unaonekana ku mkaa vyema!!! Hana cheep skendo na ni unique
3. ELIZABETH MICHAEL (LULU)
Huyu ni msanii wa bongo muvie aliye anza toka akiwa mdogo na kupata mafanikio makubwa kupitia tasnia hiyo ya bongo muvie! Ni mjasiriamali, mfanya bishara mwenye mafanikio makubwa sana kupitia tasnia hiyo ya filamu!!! Moja ya filamu zilizo mpa umaarufu sana kwa sasà nikama vile FOOLISH AGE na nyinginezo nyingi. Ana mvuto wa kipekee ambao ni uniq na classick.
2. HAMISA MOBETO
Ni mwana mitindo (model) video queen wanyimbo mbali mbali za bongo flavour!!! Ukimtazma uchoki kumwangalia she is natural sex and beauty!!! 😍 less scandel and strong
1. JOKATE MWEGELO
Aliwahi kuwa miss tanzania namba 2, ni mwanamuziki, mwana mitindo na mjasiria mali! Mfanya biashara mwenye mafanikio, mbunifu na very strong!!! Despite scandals ameweza kupata mafanikio na heshima kwa jamii!!! Ana mvuto wa kipekee (natural beauty) anayo itumia kama brand name yake kwa bidhaa zake (KIDOTI)
Hizo ni top 5 za celeb wa kike Tanzania wenye mvuto wa kipekee! Uskose the most top 5 celebs wa kike bongo wenye mkwanja mrefuuuu next tyme
MKONO ADVOCATES NA TRA
Mamlaka ya mapato Tanzania, kitengo cha walipa kodi wakubwa wamezuia mali za kampuni ya uwakili ya Mkono kwa kudaiwa kodi yenye thamani ya shilingi za kitanzania Zaidi ya bilioni moja.
TRA imetuma barua kwa kampuni ya minada ya Yono na jeshi la polisi ili kuzuia mali za kampuni ya mkono na kuziuza au kuziweka kwenye mnada ili kufidia kodi na gharama zote za usumbufu kulingana na sharia ya kodi.
TAMKO LA TRA NA VAT YA ASILIMIA 18
Press Conference imemalizika hapa TRA makao Makuu.
Kwakifupi ni kwamba Serikali imezuia Benki kupandisha viwango vya tozo katika miamala yake na kuelekeza gharama hizo kwa wateja wao.
Kamishna Mkuu wa TRA, Alphayo Kidata amesema kuwa asilimia 18 ya VAT mpya iliyopitishwa kwenye miamala ya benki inahusisha gharama zilizokuwa zikitozwa na benki hizo kwa wateja wao lakini serikali ilikuwa haipati chochote.
Kidata amesema kuwa Benki Kuu imeelekezwa kudhibiti benki hizo kwa kufanya ujanja wa kuongeza makato kwenye miamala ya wateja wao wakati wakijua fika kuwa hilo si lengo la kodi hiyo mpya.
Ameelekeza kuwa kiwango cha kodi kinachotozwa kwenye miamala hiyo kinatakiwa kubaki kama mwanzo lakini serikali itakata kodi yake ya asilimia 18 na kodi nyingine zilizopo kwa mujibu wa sheria
C&P